Monday, May 9, 2016

Rais Magufuli aamua kufanya hivi baada ya sakata la sukari kuendelea kuwaumiza wananchi Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli amesema badala ya kuwapa wafanyabiashara leseni ya kuagiza sukari kutoka ng’ambo, serikali yenyewe ndio itaagiza sukari hiyo moja kwa moja...

Msikilize..

@ ELIMU NI MUHIMU KWA WOTE, msikilize jamaa huu anavyo toa somo



Rais Dkt Magufuli ashiriki ibada ya Jumapili ya Kupaa kwa Bwana Mkoani Arusha

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ameshiriki ibada ya Jumapili ya Kupaa kwa Bwana katika Parokia ya Toleo la Bwana jimbo la Arusha leo Mei 8, 2016.
n4k64pe
 ar9
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiagana na Padri Kiongozi Germin Longio...

Saturday, May 7, 2016

Mwalimu apigwa kofi na afisa elimu


CHAMA cha Walimu (CWT) Rukwa, kimemkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga, Mathew Sedoyeka ushahidi wa maandishi unaoelezea kitendo cha Ofisa Elimu, Shule za Msingi katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga, Peter Fusi, kumshambulia na kumpiga makofi mwalimu mwenzao akiwa darasani.
 
Ushahidi huo ulikabidhiwa kwa Mkuu wa wilaya na Mwenyekiti wa CWT Mkoa wa Rukwa, Hance Mwasajone.
 
Ushahidi huo wa kimaandishi wa tukio hilo umeandikwa na mwalimu mwenyewe, Jacob Msengezi (25) ambaye alisema alipigwa mbele ya wanafunzi wake akiwa darasani shule ya msingi Kianda kabla ya kuamuru walimu wengine kufanya usafi kwa kuokota mbigili ‘miba’ iliyotapakaa katika eneo la shule hiyo akidai kuwa huo ni uchafu.
 
Sedoyeka aliwaruhusu viongozi hao kumtembelea mwalimu na kusisitiza kuwa anafuatilia kwa karibu mkasa huo ili sheria ichukue mkondo wake

Bidhaa ya sukari yaadimika nchini Tanzania

Bidhaa ya sukari imeandimika nchini Tanzania, hii imeifanya serikali Sikivu ya Tanzania inayo ongozwa na Rais Dr. JPM kuagiza kufanyika kwa uchunguzi kwa wafanya biashara wanaficha bidhaa hiyo.

Picha hapo juu inaonesha watu wakisubiri sukari katika duka moja hapa jijini Dar.
May 06 2016 Rais Magufuli alizungumza na wananchi kwa nyakati tofauti katika mikoa ya Singida na Manyara wakati waliposimamisha msafara wake uliokuwa ukitoka Dodoma kwenda Arusha. Rais Magufuli alitoa maagizo kwa wafanyabiashara wanaoficha sukari kuanza kuisambaza mara moja, vinginevyo serikali itachukua hatua kali.

Sasa taarifa iliyotolewa leo jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Valentine Mlolowa  kuwa Taasisi hiyo imeanza uchunguzi dhidi ya suala hilo kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi. 

TAKUKURU ilitembelea Maghala ya mfanyabiasha Haruni Daudi Zacharia ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Al-Naeem yaliyoko Mbagala na Tabata ambaye ni miongoni mwa wafanyabiashara wakubwa wa sukari hapa nchini na anayetuhumiwa kuficha bidhaa hiyo, haya ndio waliyoyabaini…..

TAKUKURU imebaini kuwepo kwa njama za dhati za kutouza sukari iliyokutwa katika maghala hayo kulikofanywa na mfanyabiashara huyo kwani hata sehemu ya Maghala ilipo sukari hiyo hapakuwa na dalili za upakiaji wa sukari hiyo ili iweze kusambazwa

Nduguye Bush asema hatompigia kura Trump

Aliyekuwa mgombea wa urais wa tiketi ya chama cha Republican nchini Marekani, Jeb Bush, amesema kuwa hatampigia kura Donald Trump katika Uchaguzi wa Novemba.

Bwana Bush alisema kuwa Trump hana tabia wala mienendo ya kuwa Rais wa Marekani.
Jeb ni mojawapo wa wanachama mashuhuri wa Republican kutanganza hadharani kuwa hatompigia kura Bwana Trump kwa sababu ya kampeni yake ya kiburi ambayo imegawanya chama cha Republican.

Mnamo Alhamisi Spika wa Bunge, Paul Ryan, alisema kuwa hatamuunga mkono mfanyabiashara huyo tajiri, ingawa atakutana naye juma lijalo. Hata hivyo Bwana Trump ameungwa mkono na mgombezi wa Urais wa zamani Bob Dole aliyeshindwa katika uchaguzi na Bill Clinton wa chama cha Democratic mwaka 1996.

Tanzania UK Diaspora Taskforce yatoa pongezi kwa Mh. Balozi Dkt. Asha Rose Migiro