Saturday, May 7, 2016

Bidhaa ya sukari yaadimika nchini Tanzania

Bidhaa ya sukari imeandimika nchini Tanzania, hii imeifanya serikali Sikivu ya Tanzania inayo ongozwa na Rais Dr. JPM kuagiza kufanyika kwa uchunguzi kwa wafanya biashara wanaficha bidhaa hiyo.

Picha hapo juu inaonesha watu wakisubiri sukari katika duka moja hapa jijini Dar.
May 06 2016 Rais Magufuli alizungumza na wananchi kwa nyakati tofauti katika mikoa ya Singida na Manyara wakati waliposimamisha msafara wake uliokuwa ukitoka Dodoma kwenda Arusha. Rais Magufuli alitoa maagizo kwa wafanyabiashara wanaoficha sukari kuanza kuisambaza mara moja, vinginevyo serikali itachukua hatua kali.

Sasa taarifa iliyotolewa leo jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Valentine Mlolowa  kuwa Taasisi hiyo imeanza uchunguzi dhidi ya suala hilo kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi. 

TAKUKURU ilitembelea Maghala ya mfanyabiasha Haruni Daudi Zacharia ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Al-Naeem yaliyoko Mbagala na Tabata ambaye ni miongoni mwa wafanyabiashara wakubwa wa sukari hapa nchini na anayetuhumiwa kuficha bidhaa hiyo, haya ndio waliyoyabaini…..

TAKUKURU imebaini kuwepo kwa njama za dhati za kutouza sukari iliyokutwa katika maghala hayo kulikofanywa na mfanyabiashara huyo kwani hata sehemu ya Maghala ilipo sukari hiyo hapakuwa na dalili za upakiaji wa sukari hiyo ili iweze kusambazwa