Saturday, May 7, 2016

Mwalimu apigwa kofi na afisa elimu


CHAMA cha Walimu (CWT) Rukwa, kimemkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga, Mathew Sedoyeka ushahidi wa maandishi unaoelezea kitendo cha Ofisa Elimu, Shule za Msingi katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga, Peter Fusi, kumshambulia na kumpiga makofi mwalimu mwenzao akiwa darasani.
 
Ushahidi huo ulikabidhiwa kwa Mkuu wa wilaya na Mwenyekiti wa CWT Mkoa wa Rukwa, Hance Mwasajone.
 
Ushahidi huo wa kimaandishi wa tukio hilo umeandikwa na mwalimu mwenyewe, Jacob Msengezi (25) ambaye alisema alipigwa mbele ya wanafunzi wake akiwa darasani shule ya msingi Kianda kabla ya kuamuru walimu wengine kufanya usafi kwa kuokota mbigili ‘miba’ iliyotapakaa katika eneo la shule hiyo akidai kuwa huo ni uchafu.
 
Sedoyeka aliwaruhusu viongozi hao kumtembelea mwalimu na kusisitiza kuwa anafuatilia kwa karibu mkasa huo ili sheria ichukue mkondo wake