Monday, May 16, 2016

Trump asema hataelewana na Cameron



Mgombea anaewania urais nchini Marekani Donald Trump ameonya kuwa henda asiwe na uhusiano mzuri sana na waziri mkuu wa Uingereza, David Cameron -- Ikiwa atakuwa rais wa Marekani. Mwezi Disemmba, Bwana Cameron alimtaja Trump kama mtu mwenye "ubaguzi, mjinga, na mwenye makosa" kufuatia kauli yake kwamba ataweka marufuku ya muda ya kuingia Marekani dhidi ya waislam. Bwana Cameron amekataa kufuta kauli zake dhidi ya Bilionea Trump , ambae anatarajiwa kuwa mgombea wa urais wa Marekani kupitia chama cha Republican katika uchaguzi wa mwezi Novemba. Akizungumza katika kituo cha televisheni cha Uingereza ITV kwa mara ya kwanza mbele ya umma tangu akosolewe Bwana Trump, alisema yeye si mjinga ama mbaguzi stupid bali ni''muunganishi". Kuhusu kauli za Bwana Cameron, Bwana Trump alisema : "yaelekea hatutakuwa na uhusiano mzuri sana, nani anajua. "natumai kuwa na uhusiano mwema na yeye, lakini inaonekana ni kama hataki kutatua tatizo."